WENZA KUTOKUKUBALI MAPUNGUFU YAO CHANZO CHA KUVUNJIKA KWA NDOA.

Category : Social | Sub Category : Education Posted on 2023-06-27 16:46:14


WENZA KUTOKUKUBALI MAPUNGUFU YAO CHANZO CHA KUVUNJIKA KWA NDOA.

Ili kupunguza mifarakano inayopeleka kuvunjika kwa ndoa,Wanandoa wamekumbushwa kuvumiliana kulingana na mapungufu yao kwa sababu hakuna mtu aliyokamilika asilimia mia kuwa na vigezo vyote wanavyotarajia.

Bi. Leyla Abubakari ambaye ni Mwanasaikolojia wa masuala ya malezi akizungumza na Radio Nuur fm katika Kipindi cha Mseto kinachorushwa na kituo hiki Jumatatu hadi alhamisi amesema siri ya kuishi na mtu wa jinsia tofauti (mume/mke) ni kumuangalia kwa  jicho  la wema katika mabaya yake na kumrekebisha kwa kauli nzuri.

“Akifanya kitu ambacho kinakukera au amekosea usimuangalie kwa jicho lake la tabia mbaya bali kubali kuwa ni mapungufu yake na unatakiwa umvumilie na kumuelekeza kwa kutumia kauli nzuri ambazo hazitamkera na wala kuona kama amedharauliwa”,amesema Bi Leyla.

Aidha Mwanasaikolojia huyo ambaye pia Mwalimu amesema kuwa wanandoa wajifunze kuacha mazoea ya kutoa siri zao nje kitu ambacho kinaweza kupoteza amani ndani ya ndoa zao.

“Kuna tabia ya wanandoa kuona ni kawaida kushitaki kwa ndugu,jamaa au marafiki kuhusu matatizo yenu ya ndani jambo ambalo huzaa kuzarauliwa au kutendwa kutokana na kutokuficha mambo yenu ya ndani ambayo yalistahili kumalizwa na wana ndoa husika bila kutafuta ushauri wa nje”,Amesema Bi. Leyla.

Utafiti unaonesha wanandoa wengi wamekuwa wakiingia kwenye ndoa huku wakiamini wale wanaokuwa nao wamekamilika na watakuwa vile ambavyo wao wanataka kitu ambacho sio sahihi kwani hujisahau kuwa wamekulia katika malezi ya familia tofauti.

Online streaming
Search
Leave a Comment:
Saidi Abdallah Chembea
at 2023-12-09 16:04:01
aise!